Nilitoka katika familia maskini watu wengi walituita tumelaaniwa. nilijua na kila mtu alijua. Kulikuwa na tatizo katika familia yangu; hakuna aliyeonekana kwenda popote. Mama yangu alipelekwa hospitali kwa toroli ambapo alifariki na babu yangu alipelekwa hospitali pia kwenye toroli alimofia, kaka yangu alikimbizwa mitaani; akawa mwendawazimu, wale watu unaowaona wamebeba gunia. Nilikusudiwa kufa kwa saratani nikiwa na umri wa miaka 30 lakini niko hapa.
Sikuambii hivi kwa sababu nahitaji huruma yako. Lakini kwa sababu vivuli hivyo vikawa ushindi wangu; Vivuli vya maumivu, vivuli vya kukataliwa, vivuli vya aibu, vivuli vya fedheha, vivuli vya ukosefu, vivuli vya laana na vivuli vya vita.
Vivuli hivi vimekuwa ushuhuda wangu. Kila kivuli nilichokabiliana nacho kilikuwa na ushindi.
Mimi ni mwanamke wa ushindi. Kupitia maumivu hayo, nimezaa vitabu 10, na makampuni 2, mimi ni mzungumzaji wa mabadiliko na mhudumu wa Mungu.
Je, safari ilikuwa na thamani yake?