Maisha ya Mwanaharamu ni riwaya inayosimulia kisa cha kijana mmoja anayezaliwa nje ya ndoa. Hii ni kulingana na mtazamo wa wanakijiji cha Deka. Kijana huyu anachukuliwa kama mlaanifu na anachukiwa na takribani kila mja katika kijiji hiki. Madhila anayoyapitia yanasababisha afe moyo hivi kwamba anaamua kujitia kitanzi katika Msitu wa Aguzi lakini Ibra, Mungu wa Kijiji cha Deka, anayaokoa maisha yake.
Nizikwe Kwetu Kiamboni ni riwaya inayochambua na kufafanua kwa undani madhila yanayoikumba nchi ya Kafila inayoongozwa na kiongozi aliye na uroho wa kutwaa mali yote ya nchi hiyo.