Lello Mmassy

Lello Mmassy

  • No ratings found yet!

Ninaapa Kwamba(I Solemnly Swear) by L...

KShs1,200.00
Rais Abubakar Bunende wa Jamhuri ya Watu wa Stanza anakula kiapo cha kuwa Rais na kuwahakikishia kuwa wakati huu serikali ya Stanza itasimama kidete kutetea rasilimali za Stanza kuwanufaisha wananchi waliogubikwa na wimbi kubwa la umaskini. Bunende anaamua kubadili baadhi ya sera na mifumo ili kutekeleza azma hiyo lakini anakuja kugundua mambo siyo rahisi hivyo alivyofikiria kwani anakutana na upinzani mzito wa ndani na nje kuzuia hayo anayotaka kufanya kwa sababu yanaingilia maslahi yao. Bunende anapojaribu kutaka kushindana nao wanamuua. Makamu wa Rais Bi. Mai Fabiola anachukua nchi huku akitaka kuendeleza sera za mtangulizi wake nae anafanyiwa jaribio la kuuawawa. Haamini, anachanganyikiwa. Afisa mmoja mwanamama wa Usalama wa Taifa aitwaye Hidaya anaamua kuingia mbele na kutafuta nini mzizi wa mauaji ya Rais Bunende na jaribio la Rais Mai. Nani anahusika ili ammalize.

Chochoro Za Madaraka(Alleys of Power)...

KShs1,200.00
Jasusi na Mwanadiplomasia nguli Joseph Kaduma ama Joe kama alivyozoeleka kuitwa akishirikiana na wenzake wanafanikiwa kumtoa madarakani Rais Sylvester Costa na hivyo kumweka mmoja wa mwenzao kuwa Rais wa Stanza, Habib Chamchua. Lakini hali inageuka kuwa tofauti na walivyokusudia, Korea Kaskazini nchi waliyoitumia kuwasaidia kutimiza azma ile ya kumtoa Rais Costa madarakani wanakuja na matakwa mazito yasiyotekelezeka.Joe na Rais Habib wanakuwa katika wakati mgumu wa ama kutekeleza takwa lile ama kuingia uadui na Korea Kaskazini. Wanaamua kutokutekeleza na hivyo kuingia kwenye msuguano mzito na Korea Kaskazini. Hali inakuwa ya sintofahamu kubwa hadi kupelekea Rais Habib kupotea Ikulu. Ni mtafutano usio wa kawaida.

Mimi Na Rais (The President and I) by...

KShs1,200.00
Joseph Kaduma, Shushushu na Mwanadiplomasia nguli anaingia katika sintofahamu kubwa kati yake na Rais Sylvester Costa wa Jamhuri ya watu wa Stanza.Joe, kama wengi walivyozoea kumuita serikalini ni muhanga kama walivyo wengi nchini humo kutokana na utawala dhalimu, usiozingatia misingi ya utawala bora na haki, uliojaa rushwa na unyanyasaji wa kila aina chini ya Rais Costa. Katika kuaminiwa kimashaka na Rais Costa, Joe anapewa kazi ya kurudisha mahusiano ya kidiplomasia kati ya Stanza na Korea Kaskazini na akiitumia nafasi hii yeye akiongoza baadhi ya marafiki zake waliopo ndani ya serikali na Idara ya Usalama wa Taifa wanaamua kujaribu kuleta mabadiliko ya kiuongozi nchini Stanza. Rais Sylvester Costa anawashtukia na hapo anaanza kuwawinda Joe na genge lake lote ili alimalize kwa kutaka kuleta usaliti dhidi yake. Joe anaingia kwenye vita kubwa ya kuokoa maisha yake, familia yake, rafiki zake na mali zake dhidi ya mkono wa Rais dhalimu Sylvester Costa. Ni ama yeye ama Rais.
delivery

QUICK DELIVERY

Swift dispatch

ONLINE PAYMENT

Multiple options

EXPERT SUPPORT

Help when you need it

WIDE VARIETY

Thousands of books

GLOBAL SHIPPING

Worldwide delivery

Shopping cart
Sign in

No account yet?

Shop
0 Wishlist
0 items Cart
My account