Showing 21–40 of 86 results

Sauti Za Washairi by Matata Hassan

KShs700.00 KShs550.00
Diwani hii ni kamilifu katika kukuza lugha ya mwanafunzi pamoja na kumtayarisha katika mtihani wake wa kitaifa. Ndani ya diwani hii, mwanafunzi atakumbana na maelekezo kamili kama vile Sifa mbali mbali za mashairi, bahari, jinsi ya kuutumia Uhuru wa mshairi, Pasona/nafsi neni, lugha ya nadhari na mengine mengi. Fauka ya hayo, mwanafunzi pia atakumbana na maswali na majibu ya mtihani wa kidato cha nne yatakayomsaidia katika kujiweka tayari na mtihani huo. Kwa kifupi, diwani hii ni chombo tosha kinachostahili kuabiriwa sio na mwanafunzi tu bali hata mwalimu anayepania kuwatayarisha wanafunzi vilivyo.

Kambi Ya Shetani by Edmond Ongeri

KShs450.00 KShs400.00
Kambi Ya Shetani ni Tamthilia inayozungumzia uozo katika jamii.

Kudra na Kevin Oyugi

KShs769.00 KShs649.00
Riwaya hii ya Kudra ni ya aina yake. Ni riwaya ambayo imeyamulika masuala ya kisasa na yanayoiathiri jamii kwa njia hasi ama chanya. Mhusika Kudra anajipata akitopea katika ukwasi wa aina yake licha ya kuzaliwa katika jamii ya ukata hohehahe. Hizi zinakuwa ni kudra za Mwenyezi Mungu au majaaliwa kama waambavyo wengine. Mbali na haya majaaliwa yake, anafikwa na mkosi pale ambapo rafiki yake wa chanda na pete Jane anafia katika chumba chake. Hii ni baada ya wao kulewa chopi na kusindikizwa kiamboni kwa Kudra na Bwana Majuto usiku uliotangulia. Je, haya ni majaaliwa pia? Kakaye Kudra, Oscar Mpimbi naye katika umasikini wake anafanikiwa kuchumbiana na Daktari Agnes aliyekuwa akimtibu mamaye kabla ya kuaga dunia. Oscar anampenda Agnes licha ya kuogopa kumjuvya hali ya hisia zake. Kwa upande mwingine, Agnes naye anampenda Oscar na kuamua kumfahamisha. Je, hii ni kudra ya Rabana pia? Utamu wa riwaya hii hauishii tu kuisoma kwa burudani ila pia kujifunza masuala ibuka na ainati katika jamii. Ni riwaya ya kizazi cha leo na uleo ndani mwake! Jipatie nakala ujifahamishe zaidi!

Walanyama na Mashairi Mengine by Ken ...

KShs800.00 KShs650.00
WALANYAMA ni diwani la mashairi yanayoonyesha taswira ya jamii ya sasa. Jamii ambayo imetawaliwa na dhulma, unyanyasaji, unafiki na jinsi mapenzi yamekosa maana kwa kuyapuuza maswala ya jadi. WALANYAMA ni nyenzo ya bahari mbalimbali za ushairi zilizoshughulikiwa kwa ukamilifu kwa manufaa ya jamii yote ya ulimwengu.

Nyumba Ya Msonge Ya Nyanya Yangu

KShs300.00 KShs230.00
Title: Nyumba ya Msonge ya Nyanya Yangu Series: Msururu wa Discovery Author: Toroitich Patrick Yegon Target Class: Early Readers grade 1-3 Hadithi hii inalenga kukuza uelewa wa watoto wa mazingira yao na kuwawezesha kutunga hadithi kuhusu vifaa, wanyama, maliasili na vitu vingine vingi wanoatumia kila siku. Hadithi hii imeandikwa kulingana na maisha ya kijijini. Inazungumza kuhusu maisha yake nyanya ya msimulizi na jinsi anavyoishi na wanajamii wengine, marafiki, wageni na pia wanyama wao.

Likizo Mashambani by Toroitich Patric...

KShs500.00 KShs350.00
Title: Likizo Mashambani Series: Hadithi za Kiafrika Author: Toroitich Patrick Yegon Target Readers: Class 5,6,7,8 Hadithi hii inasimulia matukio aliyoyapitia Shani alipozuru kijijini Kaplelekwo wakati wa likizo ya Aprili. Katu Maishani Shani hakuwahi kutarajia kuwa angewahi lia kwa kuondoka Kaplelekwo kama alivyofanya siku hiyo alipokuwa akienda kuabiri gari lililokuwa likimngoja.