Showing 21–40 of 96 results

Kengeza La Jasiri By Shisia Wasilwa

KShs749.00 KShs699.00
Jasiri ana Kengeza. Kengeza hilo halimpi amani. Linamsumbua maishani. Hilo kengeza linayaunganisha maisha yake ya zamani na usasa. Kalipata ujanani. Amekataa kulizika katika kaburi la sahau. Je, Jasiri atapata tiba ya kengeza hilo analopenda, kulificha pembeni mwa kijoyo chake? Anagundua pia marehemu babake kaaga dunia kutokana na hilo kengeza. Je, haya makengeza ndiyo nini? Ni masimulizi yanayonata, yaliyosheheni taharuki na maudhui mazito. Kuhusu mwandishi Shisia Wasilwa ni mwandishi na mwanahabari stadi wa siku nyingi. Aliwahi kuhudumu na Shirika la Habari nchini Kenya-KBC, China Radio Kimataifa, Citizen Tv na Radio, BBC na Deutsche Welle-DW. Baadhi ya kazi zake ni pamoja Makovu ya Uhai na Dunia Tambara Bovu. Alihariri Ndoto ya Almasi chake Ken Walibora, mwongozo wa Utengano wa Said. A. Mohammed miongoni mwa kazi nyingine teule. Kwa sasa anazamia shahada ya uzamili katika masuala ya mawasiliano katika chuo Kikuu cha Aga Khan.

Walanyama na Mashairi Mengine by Ken ...

KShs800.00 KShs650.00
WALANYAMA ni diwani la mashairi yanayoonyesha taswira ya jamii ya sasa. Jamii ambayo imetawaliwa na dhulma, unyanyasaji, unafiki na jinsi mapenzi yamekosa maana kwa kuyapuuza maswala ya jadi. WALANYAMA ni nyenzo ya bahari mbalimbali za ushairi zilizoshughulikiwa kwa ukamilifu kwa manufaa ya jamii yote ya ulimwengu.

Nyumba Ya Msonge Ya Nyanya Yangu

KShs300.00 KShs230.00
Title: Nyumba ya Msonge ya Nyanya Yangu Series: Msururu wa Discovery Author: Toroitich Patrick Yegon Target Class: Early Readers grade 1-3 Hadithi hii inalenga kukuza uelewa wa watoto wa mazingira yao na kuwawezesha kutunga hadithi kuhusu vifaa, wanyama, maliasili na vitu vingine vingi wanoatumia kila siku. Hadithi hii imeandikwa kulingana na maisha ya kijijini. Inazungumza kuhusu maisha yake nyanya ya msimulizi na jinsi anavyoishi na wanajamii wengine, marafiki, wageni na pia wanyama wao.

Likizo Mashambani by Toroitich Patric...

KShs500.00 KShs350.00
Title: Likizo Mashambani Series: Hadithi za Kiafrika Author: Toroitich Patrick Yegon Target Readers: Class 5,6,7,8 Hadithi hii inasimulia matukio aliyoyapitia Shani alipozuru kijijini Kaplelekwo wakati wa likizo ya Aprili. Katu Maishani Shani hakuwahi kutarajia kuwa angewahi lia kwa kuondoka Kaplelekwo kama alivyofanya siku hiyo alipokuwa akienda kuabiri gari lililokuwa likimngoja.